Monday, May 28, 2018

MHE DKT ANGELINE MABULA AUNGANA NA WABUNGE WENGINE KUSAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO KIFO CHA MHE KASUKU BILAGO

Mbunge wa Jimbo la Ilemela na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe Dkt Angeline Mabula ameungana na waheshimiwa wabunge wengine wakiongozwa na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Tulia Ackson pamoja na mke wa aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa awamu ya nne Mhe Salima Kikwete katika kusaini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Buyungu kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Mhe Mwl. Kasuku Samson Bilago kilichotokea juzi katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili Jijini Dar es Saalam alipokuwa akipatiwa matibabu.

Aidha kwa  siku ya Kesho Jumanne ya  Mei 29, 2018 wabunge wote watapata fursa ya kuaga mwili wa marehemu katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma.
' Bwana ametoa, Bwana ametwaa, Jina la Bwana lihimidiwe '




No comments:

Post a Comment