Friday, April 12, 2024

Baraza kuu la waisilamu Tanzania (BAKWATA) Mkoa wa Singida imemtunuku cheti cha pongezi Ndg. Ahmed Misanga

BismillahI alrahmani alrahim. 

Baraza kuu la waisilamu Tanzania 🇹🇿 (BAKWATA) Mkoa wa Singida  imemtunuku cheti cha pongezi Ndg. Ahmed Misanga kwa Kuendelea Kutoa Mchango wake kwa Watu wenye uhitaji Katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhan,Ndg.Ahmed Misanga aliongoza RAMADHAN CHARITY PROGAMME 2024 , na kufikia zaidi ya Wahitaji 1500.  

JAZAKALLAH KHEIR






Thursday, April 28, 2022

RAMADHAN CUP 2022 KANKONO AJIVUNIA VIPAJI VYA VIJANA VILIVYOKO MKOA WA MWANZA

Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Mkoa wa Mwanza Ndugu Dennis Nyamlekela Kankono amesema Mkoa wa Mwanza unaongoza kwa kuwa na Vijana wengi wengi wenye vipaji Mbalimbali kama Soka,Filamu,Waimbaji,Waigizaji n.k.

"Mkoa wa Mwanza katika Soka tunaitwa Brazil sababu kutoa wachezaji wengi kama Calvin Yondani, Enry Joseph, Mrisho Ngasa, Mwinyi Kazimoto n.k."

aneyasema katika Mchezo wa Nusu fainali ya pili ya Mashindano ya Ramadhani Cup ambayo yamedhaminiwa na Mhe. Stanslaus Mabula (MB) bado yameendelea leo na ambapo Mgeni Rasmi katika nusu fainali hii alikuwa Katibu wa UVCCM Mkoa wa Mwanza Ndg. Dennis Nyamlekela Kankono.

katika Mchezo huo Timu ya Mwanza mjini imeibuka kidedea kwa ushindi wa magoli mawili kwa moja.

Fainali ya Ramadhan Cup itakuwa Ijumaa ya tarehe 29/04/2022.

USIKOSE! 







KINANA ATAKA WALIOTAJWA RIPOTI YA CAG HATUA ZICHUKULIWE.

 MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana ametoa ushauri kwa Serikali kuhakikisha wote waliotajwa kufuja fedha za umma kwenye ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali(CAG) wanachukuliwa hatua.

Amesema haina maana kila mwaka ripoti ya CAG inatolewa halafu hakuna hatua ambazo zinachukuliwa dhidi ya wahusika wote ambao wametajwa, hivyo umefika wakati sasa kuchukua hatua ili kukomesha ufujaji wa fedha za umma.

“Kumekuwa na matumizi mabaya ya fedha za umma kinyume na utaratibu, niwoambe wenzangu serikali, ni wakati muafaka watu waliotajwa, waliohusika, waliotenda, walioshiriki kwa namna moja au nyingine wachukuliwe hatua.

“Wakati umefika kwa Serikali kufanyia kazi kwa kina ripoti ya CAG ili wananchi waridhike mali ya umma haitumiki vibaya.Mnaunga mkono au tuwahurumie, haiwezekani vitabu vya CAG vinaandikwa kila mwaka hali inakuwa hivyo hivyo , lazima tuchukue hatua, uamuzi wa kuagiza serikali sina lakini uwezo wa kushauri ninao,”amesema Kinana.





Saturday, April 23, 2022

KATIBU WA UVCCM (W) YA ILEMELA AENDELEA KUCHANJA MBUGA

 Mapema Leo katibu wa UVCCM( W) ya Ilemela Ndugu HAMISI MAGOHE  ameendelea na Ziara yake katika kata ya Kahama na Shibula


Katika ziara hiyo aliyoambatana na Katibu wa Uhamasishaji na Chipukizi Ndugu Edwine Kabide ,katibu huyo amezidi kutoa maelekezo mablimbali yanayohusu uchaguzi na zoezi la uchukuaji na urejeshwaji wa fomu katika matawi 

Akizungumza na vijana pamoja na makatibu wa CCM wa matawi mbalimbali ,katibu amewakusha Viongozi wa jumuiya ya vijana kuhakikisha kuwa wanasimamia kanuni ,muongozo na taratb mbalimbali za Chama na jumuiya yake ili kufanikisha zoezi la uchaguzi kwenda Kwa haki na uwazi 

Pamoja na mambo mengine ,katibu huyo ametumia nafasi hiyo kuwakumbusha vijana kujitokeza Kwa wingi na kutoa Hamasa Kwa wananchi katika maeneo Yao kujitokeza Kwa wingi ili waweze kuhesabiwa pindi zoezi hilo la sensa litakapofika 

#Kazi iendelee
#Ilemela kazini
#Viva Vijana Viva 
#Alipo Mama ,vijana tupo







DR ANGELINE SL MABULA KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 100 YA HAYATI J K NYERERE

 Mapema Leo Waziri wa Ardhi ,Nyumba na maendeleo ya makazi DR ANGELINE SL MABULA ( MB) wa Jimbo la Ilemela ameshiriki katika maadhimisho ya miaka 100 ya Hayati JK Nyerere 


Katika maadhimisho hayo yaliyohudhuliwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali wameaswa kuyaishi na kuyaendeleza mema yote aliyoyafanya Hayati JK Nyerere enzi za uhai wake 

#Kazi iendelee
#Nshimba Nkema kazini 
#Ilemela ni yetu tushirikiane kuijenga


ILEMELA YANG'ARA TUZO ZA USIMAMIZI BORA WA MIRADI YA AFYA NA ELIMU MKOA WA MWANZA

 Wilaya ya Ilemela imeibuka kidedea katika tuzo za usimamizi bora wa miradi ya afya na elimu zilizotolewa na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe Mhandisi Robert Gabriel kwa wilaya zote za mkoa  huo.



Wilaya ya Ilemela imefanikiwa kutwaa tuzo ya usimamizi bora wa miradi ya afya kwa kuwa mshindi wa kwanza, tuzo ya mshindi wa pili mitihani ya kidato cha pili kitaifa kwa mwaka 2021, tuzo ya mshindi wa kwanza mitihani ya kitaifa kwa darasa la nne kwa mwaka 2021 ambapo mkuu wa mkoa wa Mwanza akazitaka halmashauri zote za mkoa huo kuweka msukumo katika kuongeza kasi ya usimamizi wa miradi ya maendeleo Kwa wananchi sambamba na matumizi sahihi ya fedha za miradi ya maendeleo zinazotolewa na Serikali

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Ilemela Mhe Hasan Elias Masalla ameshukuru Kwa wilaya yake kufanikiwa kutwa tuzo hizo huku akiahidi kuongeza kasi katika kuisimamia wilaya yake katika kutekeleza miradi yenye tija Kwa wananchi itakayozingatia mahitaji ya wakati na thamani ya fedha

Zoezi la utoaji wa tuzo hizo lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka wilaya zote za mkoa wa Mwanza wakiwepo wakuu wa wilaya, wakurugenzi, mameya na wenyeviti wa halmashauri.












Thursday, April 21, 2022

DKT MABULA AKABIDHI SADAKA YA FUTARI KWA TAASISI ZA ELIMU JIMBO LA ILEMELA

 Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mhe Dkt Angeline Mabula Leo amekabidhi sadaka ya futari Kwa  taasisi za Elimu zilizopo ndani ya Jimbo hilo ikiwemo shule ya sekondari Bwiru wavulana, Chuo Cha Mipango na shule ya sekondari Bwiru wasichana ambapo Sukari Kilo 110 zilitolewa Kwa kila taasisi, Mchele Kilo 110 kwa Kila taasisi, Tambi na Tende Ili wanafunzi waislamu waweze kupata futari katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhan


Akizungumza wakati wa makabidhiano ya sadaka hiyo, Katibu wa Mbunge Ndugu Kazungu Safari Idebe amesema kuwa Mbunge wa Jimbo la Ilemela amekuwa na utaratibu wa kuungana na waumini wa dini ya kiislamu kila mwaka unapofika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan kwa kutoa sadaka ya futari ili kusaidia waumini hao waweze kufunga kwa salama na amani 

'.. Mhe Mbunge alitamani kuwepo yeye mwenyewe katika zoezi hili, Lakini kutokana na majukumu ya kitaifa aliyopewa ameshindwa ingawa siku za hivi karibu alianzisha yeye mwenyewe zoezi hili Kwa kutoa sadaka hii katika vituo vya watoto yatima, Wajane, Misikiti, Wazee na Watu wenye uhitaji, Na leo sisi wasaidizi wake akaamua tumuwakilishe kuendelea alipoishia..' Alisema

Aidha Ndugu Kazungu amefafanua kuwa Serikali na nchi Kwa ujumla  ina mategemeo makubwa Kwa wanafunzi hao na kuwaasa kuutumia mwezi huu mtukufu kuombea taifa na viongozi wake wakiongozwa na Rais Mhe Samia Suluhu Hassan sanjari na kuongeza kuwa taifa lolote lenye hofu ya Mungu lazima liwe na Maendeleo 

Kwa upande wake Mkuu wa shule ya sekondari Bwiru wasichana Mwalimu Mektilda Shija mbali na kumshukuru Mbunge huyo amesema kuwa Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mhe Dkt Mabula amekuwa mtu wa msaada katika shule yake na si mara ya kwanza kufika kutoa misaada kwani mara kadhaa amekuwa akishirikiana nao katika kutatua kero mbalimbali zinazoikabili shule hiyo hivyo kuwataka wanafunzi wake kumuombea hasa katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhan

Hawa Japhari ni mwanafunzi wa kidato Cha Tano anaesoma masomo ya mchepuo wa sayansi (CBG) katika shule ya wasichana Bwiru amempongeza na kumshukuru Mbunge Mhe  Dkt Angeline Mabula Kwa msaada alioutoa pamoja na kumuombea Kwa Mungu Ili kidogo alichokitoa aweze kuzidishiwa





Thursday, December 23, 2021

ZIARA YA KAMATI YA SIASA MKOA WA MWANZA YA KUKAGUWA UJENZI WA MADARASA

 Kamati ya siasa mkoa wa Mwanza chini ya Mwenyekiti Dr Antony Diallo  ilijigawa katika makundi matatu  kwa lengo la kukaguwa ujenzi wa Madara ya Fedha za UVIKO19 zilizotolewa na Rais wa awamu ya Sita  Samia Suluhu Hassan mama wa Vitendo

Kundi lililo ongozwa na Mnec  Jamal Babu na Mwenyekiti UWT (M) Ma Helen Bogohe ,Katibu jumuiya ya wazazi  Zamda kamugisha na katibu wa Uhamasishaji na Chipkizi UVCCM (M) Ndugu Hussein A Kimu walitembelea wilaya ya Kwimba

Katika ukaguzi huo Mnec  Jamal Babu amewataka viongozi wanao simamia miradi hiyo ya ujenzi wa madarasa kukamilisha kwa mda uliopagwa na kuendelea kuhakikisha ubora na usimamizi wa fedha hizo