Wilaya ya Ilemela imeibuka kidedea katika tuzo za usimamizi bora wa miradi ya afya na elimu zilizotolewa na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe Mhandisi Robert Gabriel kwa wilaya zote za mkoa huo.
Wilaya
ya Ilemela imefanikiwa kutwaa tuzo ya usimamizi bora wa miradi ya afya
kwa kuwa mshindi wa kwanza, tuzo ya mshindi wa pili mitihani ya kidato
cha pili kitaifa kwa mwaka 2021, tuzo ya mshindi wa kwanza mitihani ya
kitaifa kwa darasa la nne kwa mwaka 2021 ambapo mkuu wa mkoa wa Mwanza
akazitaka halmashauri zote za mkoa huo kuweka msukumo katika kuongeza
kasi ya usimamizi wa miradi ya maendeleo Kwa wananchi sambamba na
matumizi sahihi ya fedha za miradi ya maendeleo zinazotolewa na Serikali
Kwa
upande wake Mkuu wa wilaya ya Ilemela Mhe Hasan Elias Masalla
ameshukuru Kwa wilaya yake kufanikiwa kutwa tuzo hizo huku akiahidi
kuongeza kasi katika kuisimamia wilaya yake katika kutekeleza miradi
yenye tija Kwa wananchi itakayozingatia mahitaji ya wakati na thamani ya
fedha
Zoezi la utoaji wa
tuzo hizo lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka wilaya zote za
mkoa wa Mwanza wakiwepo wakuu wa wilaya, wakurugenzi, mameya na
wenyeviti wa halmashauri.
No comments:
Post a Comment