Wednesday, June 27, 2018

TANZIA.. TANZIA.. Mhe Dkt Angeline S.L Mabula amepokea kwa mshtuko mkubwa

Mbunge wa Jimbo la Ilemela ambae pia ni Naibu Waziri wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe Dkt Angeline S.L  Mabula amepokea kwa mshtuko mkubwa na masikito taarifa za kifo cha aliyekuwa Diwani wa Viti maalum manispaa ya Ilemela kupitia chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) Mhe Dotto Ponsian Balilemwa wa kata ya Nyamanoro.

Aidha Mhe Mbunge anawapa pole ndugu, jamaa, marafiki, wananchi wote, viongozi wa chama na serikali walioguswa na msiba huo huku akiwataka kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mpendwa wao.

' Bwana ametoa, Bwana ametwaa, Jina la Bwana lihimidiwe '

Imetolewa na
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Ilemela
27.06.2018

No comments:

Post a Comment