Rais
Dkt. John Magufuli amepokea kwa mshtuko na masikitiko taarifa ya vifo
vya watu 14 waliopoteza maisha baada ya basi dogo walilokuwa wakisafiria
kugongana uso kwa uso na lori la kubebea mchanga katika eneo la Dundani
Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani.
Dkt.
Magufuli amesema hayo katika salamu zake za rambirambi kwa Mkuu wa Mkoa
wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo baada ya kupita masaa kadhaa tokea
ajali hiyo kutokea leo Juni 25, 2018 wakati basi dogo lililowabeba
wanafamilia, ndugu na jamaa waliokuwa wakielekea Msata kuhudhuria
sherehe za kumaliza mafunzo ya kijeshi kwa mtoto wao, kugongana uso kwa
uso na lori lililokuwa linatoka Dar es Salaam kwenda Dundani kuchukua
mchanga.
"Naomba
unifikishie pole nyingi kwa wanafamilia wote waliopatwa na msiba,
waambie naungana nao katika kipindi hiki kigumu cha majonzi ya
kuondokewa na wapendwa wao, na sote tuwaombee marehemu wote wapumzishwe
mahali pema peponi", amesema Rais Magufuli.
Kwa
upande mwingine Rais Magufuli pia amewaombea majeruhi wanne wa ajali
hiyo wapone haraka ili waweze kuungana na familia zao na kuendelea na
majukumu yao ya kila siku.
No comments:
Post a Comment