Wananchi wa Jimbo la Ilemela mkoani Mwanza wametakiwa
kujitoa kwa kuchangia damu ili kuokoa maisha ya watu wengine sambamba na
kujiwekea akiba pindi unapotokea uhitaji kwao binafsi.
Hayo yamesemwa leo na Mbunge wa Jimbo la Ilemela ambae pia
ni Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe Dkt Angeline
Mabula wakati wa Uzinduzi wa mradi wa Uthamini wa bidhaa za nyumbani
uliyopewa jina la HOME KWANZA uliohusisha makundi ya Vijana wazalishaji
wa bidhaa mbalimbali na wasanii wa maigizo, muziki, uchoraji kwa
kuonyesha shughuli zao na kisha kuchangia Damu katika kuokoa maisha na
kuunga mkono jitihada za Serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais Mhe Dkt
John Magufuli.
Aidha Mhe Dkt Angeline Mabula ameongoza Vijana
waliojitokeza katika Uzinduzi huo kwa yeye kuchangia Damu sambamba na
kufafanua juu ya umuhimu wa kuchangia Damu mbali na kuokoa maisha
akitaja kujua afya zao na kujiepusha na magonjwa yanayotokana na kuzidi
kwa Damu mwilini.
Kwa upande wake muwakilishi kutoka Damu Salama ndugu
Emanuel Ndaki amewahakikishia wananchi waliojitokeza katika kuchangia
Damu kuwa zoezi hilo linaendeshwa kitaalamu hivyo hawapaswi kuwa na hofu
yeyote na taarifa zote zinabaki kuwa siri.
Akihitimisha muasisi wa Mradi wa Home Kwanza na mmiliki wa
White Fish Entertainment Ndugu Frank Nubi mbali na kumshukuru Mhe Dkt
Angeline Mabula kwa kuwaunga mkono na ushiriki wake wa tangu kuasisiwa
kwa mradi huo amemuomba Mbunge huyo kuendelea kuwaunga mkono Vijana
katika kutumia Vipaji vyao kwa kuleta maendeleo na kujikwamua kiuchumi
sambamba na kuthamini bidhaa zinazozalishwa nyumbani.
‘Ilemela ni yetu, tushirikiane kuijenga’
Imetolewa na
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Ilemela
29.10.2017
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Ilemela
29.10.2017




No comments:
Post a Comment