Tuesday, February 6, 2018

Mamlaka ya hali ya hewa yatoa tahadhari kwa wakazi wa Dar, Pwani na Tanga

Mamlaka ya hali ya hewa nchini Tanzania (TMA) imetoa tahadhari kwa wananchi kuwepo kwa hali mbaya ya hewa katika maeneo yote ya pwani kuanzia leo(jana) usiku mpaka Februari 7 mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana Februari 05, 2018 kutakuwa na vipindi vifupi vya upepo mkali unaozidi kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayozidi mita 2 ambavyo vinatarajiwa katika maeneo ya mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani, Lindi na Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba. 

No comments:

Post a Comment