Tuesday, February 13, 2018

MWENYEKITI UVCCM TAIFA COMRADE KHERI D JAMES AWAFUNDA WANA MISUNGWI

MWENYEKITI UVCCM TAIFA COMRADE KHERI D JAMES AWAFUNDA WANA MISUNGWI

Mwandishi Hussein A. Kimu

Mwenyekiti wa umoja wa vijana Taifa Comrade Kheri D James leo tarehe 13/2/2018 katika kata ya kanyerere wilaya ya misungwi mkoa wa mwanza amewafunda mamia ya wananchi walio hudhuria katika mkutano wa hadhara  wa kumunadi mgombea  udiwani wa chama cha mapinduzi ndugu Daniel .

Mwenyekiti wa umoja wa vijana Taifa alianza kwa kufikisha salamu za Mhe Rais wa Jamuhuri ya muungano na mwenyekiti wa chama cha mapinduzi Taifa Dr John Pombe Magufuli

Kwakuwambia Rais wetu  anawapenda sana wana kanyerere wana misungwi na watanzania wote
Rais wetu mpendwa amejitoa kwa ajili ya watanzania wote wapenda maendeleo hasa wanyonge wote tuendelee kumuombea na kumuunga mkono .

Mwenyekiti aliwafunda wana misungwi kwa kueleza faida za kumuchagua mgombea anaetokana na chama cha mapinduzi

Pia mwenyekiti aliwaomba wananchi walio hudhuria mkutano huo kuendelea kukiamini chama cha mapinduzi na serikari yake mana ndio wenye jukumu la kweli la kuleta mabadiliko yenye tija kwa watanzania

Mkutano huo ulihudhuriwa na viongozi wa chama na jumuiya zake ngazi ya  wilaya mkoa na wabunge akiwemo Mbunge wa Ji mbo la Nyamagana Mhe Stanislaus Mabula

TUKUTANE KAZINI 



No comments:

Post a Comment