Baada ya Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi hapa nchini (TSNP), Abdul
Nondo aliyepotea usiku wa kuamkia March 7, 20018 katika mazingita
kutatanisha, kuonekana akiwa mkoani Iringa
Jeshi la Polisi Mkoani humo
limeibuka na kusema limefungua jalada ili kuchunguza mazingira ya
upoteaji wa Nondo.
Akizungumza na wanahabari mapema leo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Iringa, Juma Bwire amesema uchunguzi huo umelenga kubaini kama Nondo
alitekwa kweli na watu wasiojulikana au alitoa taarifa za uongo.
Amesema, Nondo ambaye pia ni Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam amepatikana akiwa hai na salama bila ya kuwa na mareha yoyote
mwilini mwake yanayoashiria alipata mateso.
Kamanda Bwire amesema hadi sasa Nondo bado yupo kituoni hapo wakati
uchunguzi unafanyika na kwamba ikibainika alitoa taarifa za uongo
atachukuliwa hatua za kisheria.

No comments:
Post a Comment