Sunday, March 4, 2018

MBUNGE JIMBO LA NYAMAGANA AWA LULU KATA YA MAHINA

Mbunge Jimbo la Nyamagana kutatua kero ya ardhi kwa Kaya 636, kuboresha sekta ya elimu, afya na miundombinu na  barabara pamoja upatikanaji wa Soko Kata ya Mahina.
Mhe Stanislaus Mabula akiongea na wananchi wa kata  ya Mahina kuelezea utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi 2015-2020. 

Amesema uongozi wake umewezesha upatikanaji wa hati za viwanja vya makazi kwa Kaya 636 ambazo zitatolewa wiki mbili zijazo baada ya mchoro wake kukamilika na  kunufaisha mitaa minne ya Kata hiyo.

Katika kuboresha sekta ya elimu mhe Mabula amewaambia wananchi amewezesha upatikanaji wa shilingi million 18,500,000 ambazo shilingi millioni 9,600,000 imeenda shule ya Nyaruguru  kumalizia ujenzi wa  darasa ambayo ina upungufu wa Vyumba vya madarasa 40. Kadharika shilingi 8,900,000 zimeenda katika ujenzi wa matundu ya vyoo  bora shule ya sekondari ya Mahina ambayo ilikuwa imekwama.


Kukabiliana na changamoto ya Maji Safi na Usalama tayari serikali ya  awamu ya  tano imewezesha ujenzi wa matank mawili yenye uwezo wakuhifadhi Lita 1,000,000  tank mmoja linaweza kuhifadhi ujazo wa  Lita 800,000  na lingine lita 200,000 na tayari mkandarasi anaendelea na Kazi.
Katika sekta ya afya amesimamia  upatikanaji wa shilingi million 78,000,000 zitakazosaidia kukamilisha wodi la  wanawake wajawazito na watoto ilikupandisha hadhi Zahanati hiyo kuwa kituo cha Afya.


Amefafanua serikali ya awamu ya tano imewezesha ujenzi wa barabara kutokea bendera tatu, Igeregele, Mahina  shule ya msingi, Bugarika hadi kufika  Bugando hospitali Kata ya Pamba ambayo iliwekewa jiwe la msingi na Mwenge wa  Uhuru 2017. Ambapo Mwaka ujao wa Fedha  barabara hiyo imitengewa Fedha kilometa 2 kwa kipande kilichobakia. Pia ujenzi wa barabara ya Mahina Kati,  Tambukareli kutokea Kata ya Mkuyuni kupunguza msongamano wa  Magari inatazamiwa kuanza.


Amemalizia kuipongeza ofisi ya mkurugenzi  wa halmashauri ya Jiji la Mwanza kwaushirikiano wake na Baraza la  madiwani kutenga fidia ya shilingi millioni 60,000,000 kulipa eneo la Kiwanja kwaajili ya ujenzi wa Soko Kata hiyo.
Imetolewa na, 


Ofisi ya mbunge, 
Jimbo la Nyamagana






No comments:

Post a Comment