Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi inaendelea
na maonesho yake ya siku tangu kuanzia Mei 28, 2018 katika viwanja vya
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mjini Dodoma yaliyokutanisha
wadau mbalimbali wa Ardhi kutoa elimu ya ardhi na mipango miji ili
kurahisisha upatikanaji wa huduma na kuzuia ujenzi holela.
Akizungumza Naibu Waziri wa Wizara hiyo na Mbunge wa Jimbo
la Ilemela Mhe Dkt Angeline Mabula mara baada ya kutembelea maonesho
hayo amesema kuwa wizara imeandaa maonesho hayo ili kuwakutanisha wadau
wa Ardhi kwa pamoja ambapo zaidi ya makampuni 30 yamehusishwa ikiwemo
Watumidhi House, Makampnu ya Waendelezaji Milki, Makampuni ya Upangaji
na Upimaji, Makampuni ya Vifaa vya Ujenzi na Mabenki yanayotoa mikopo ya
Nyumba
‘… Kama wizara tumeandaa maonesho yatakayowakutanisha wadau
mbalimbali wa ardhi kabla ya kuwasilisha bajeti yetu, nitumie firsa hii
kuwaomba waheshimiwa wabunge, wageni waalikwa na watumishi wa bunge
kutembelea maonesho hayo ili kufahamu mambo mengi juu ya ardhi …’
Alisema
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi inatarajia
kuwasilisha leo bajeti yake kwa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania kwa mwaka wa fedha 2018/2019 ili wabunge waweze kuijadili
na kutoa mapendekezo yao na kisha kuipitisha.
No comments:
Post a Comment