Jamii imeaswa kuwafichua na kuwasaidia watoto walemavu ili
waweze kupata huduma muhimu za afya na elimu zitakazowasaidia kufikia
ndoto zao
Kauli hiyo imetolewa leo na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa
Mwanza kupitia kundi la vijana (UVCCM) Mhe Maria Kangoye wakati
akizungumza na viongozi na wanachama wa chama cha mapinduzi kata ya
Kirumba wilayani Ilemela alipokuwa akikabidhi jumla ya baiskeli 25 kwa
walemavu wa mkoa wa Mwanza ambapo ameiasa jamii kutowaficha walemavu na
kuwakandamiza katika kutimiza malengo yao.
‘… Imefika hatua tunataka kuliona suala la ulemavu kama
jambo la kawaida, tumeshuhudia wakifichwa majumbani, tumeshuhudia
wakikosa fursa mbalimbali kutokana na hali zao, wengi wamekuwa hata
wakipelekwa mashuleni wanarudishwa …’ Alisema
Aidha Mhe Kangoye amempongeza na kumshukuru Mbunge wa Jimbo
la Ilemela Mhe Dkt Angeline Mabula kwa namna anavyoshirikiana nae
katika kuhakikisha wanawatumikia wananchi kwa kutatua kero zao sambamba
na kuwataka wanachama hao kueleza mazuri yanayofanywa na Serikali ya
chama cha mapinduzi chini Mhe Rais Dkt John Magufuli na wasaidizi wake.
Nae Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) wilaya ya
Ilemela Ndugu Salome Kipondya amemshukuru mbunge huyo kwa uamuzi wake wa
kusaidia watoto walemavu wa wilaya yake huku akimuahidi ushirikiano
katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM na kuwaletea wananchi
maendeleo..
Kwa wilaya ya Ilemela watoto Brenda Kennedy mwenye umri wa
miaka 17 anaesoma mpango wa elimu ya watu wazima, Eric Ngembe mwenye
umri wa miaka 14 mkazi wa Kirumba anaesoma Sunrise sekondari na Kelvin
Razaro mwenye umri wa miaka 5 mkazi wa Buzuruga anaesoma shule ya awali
wamemshukuru mbunge huyo kwa kunufaika na baiskeli hizo za walemavu
alizozitoa zitakazowasaidia katika maisha yao ya kila siku.
Zoezi hilo la ugawaji wa baiskeli kwa watoto walemavu
lilishuhudiwa pia na mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mwanza, Katibu wa CCM
wilaya ya Ilemela, na madiwani wa viti maalum wa wilaya hiyo.
No comments:
Post a Comment