Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeandika
historia mpya mara baada ya bajeti yake kuungwa mkono na waheshimiwa
wabunge wote pasipo wabunge hao kuzuia shilingi kama ilivyokuwa siku za
nyuma ikiwa ni wizara yenye kukosolewa na kila mbunge aliyesimama
kuchangia hoja badala yake wabunge wamepongeza waziri na naibu waziri
wa wizara hiyo pamoja na watendaji wao kwa mafanikio iliyoyapata na
kuonyesha mwanga wa kufanya vizuri zaidi kwa kubaini mwarobaini wa
kumaliza migogoro ya ardhi, kupanga miji na kusimamia mapatao
yanayotokana na sekta hiyo.
Kwa mwaka wa fedha 2018/2019 Wizara hiyo imetenga kiasi
cha fedha jumla ya shilingi 79 Bilioni na kupitishwa na kikao cha 40 cha
Bunge la Bajeti chini ya Mwenyekiti wa kikao hicho Mhe Mussa Azzan
Zungu.
Aidha wakichangia wakati wa uwasilishwwaji wa bajeti hiyo
wabunge tofauti tofauti mbali na kupongeza Waziri wa Wizara hiyo Mhe
William Lukuvi na Naibu Waziri wake Mhe Dkt Angeline Mabula wametaja
mambo mbalimbali yaliyokuwa yakiwasumbua wananchi ambayo sasa mara baada
ya kupitishwa kwa bajeti hiyo yataenda kupata suluhu ya kudumu wakitaja
migogoro ya ardhi na upatikanaji wa hati.
No comments:
Post a Comment