Wednesday, June 12, 2019

ZIARA YA KAMATI YA UTEKELEZAJI UVCCM MKOA WA MWANZA YALETA UFANISI KWA VIJANA WA WILAYA YA UKEREWE

Mapema leo tarehe 12/6/2019

Mwenyekiti wa umoja wa vijana mkoa wa mwanza Comrade Jonas Lufungulo
aliwaongoza wajumbe wa kamati ya UTEKELEZAJI ya umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi wilani UKEREWE

Ziara hiyo imelenga kukutana na mabaraza yote ya kata katika maeneo yao au katika kata zao husika

ikiwa lengo ni
Kukaguwa uhai wa jumuiya,
kuwahamasisha vijana na wana ccm wote kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa serikali za mitaa 2019

kuwajengea uwezo wa kiuchumi vijana kwa kuwaelekeza kujituma katika kufanya kazi na kuunda vikundi vya ujasilia mali ,kuwa wabunifu (creativity)

Kuunga mkono jitiada za mwenyekiti wa chama cha mapinduzi Taifa  Dr Josefu Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anazo zifanya za kuwatumikia watanzania wote kwa moyo wa uzalendo

Nae mtendaji mkuu wa jumuiya mkoa wa mwanza Comrade Denis Luhende amehimiza kwa vijana wa ccm kuwa na utii wa bila shuruti pindi wanapopewa  maelekezo na viongozi wao

katika ziara hiyo vijana wamejitokeza kwa wingi na kutowa kero zao na changamoto zinazo wakabili na kutolewa ufumbuzi jambo ambalo limewapa faraja kubwa sana na kutowa pongezi kwa ziara hiyo ya viongozi wa jumuiya ya vijana mkoa wa mwanza

KATIBU WA UHAMASISHAJI ,CHIPKIZI,SERA NA UTAFITI
UVCCM MKOA WA MWANZA

HUSSEIN A KIMU
TUKUTANE KAZINI


















No comments:

Post a Comment