Wednesday, September 19, 2018

ANTHONY MAVUNDE AFUNGA SEMINA YA UJASIRIAMALI LEO .


Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mhe Anthony Mavunde amefunga  Semina ya Ujasiriamali leo tarehe 19/9/2018 ambayo imeendeshwa kwa muda wa siku tatu tangu Tarehe 17/9/2018.

Kabla hajafunga mafunzo hayo Mgeni Rasmi Mh Anthony Mavunde Amempongeza M/Kiti wa UVCCM Mkoa wa MwanzaMh.Jonas Lufungulo  na kamati yake nzima kwa kuandaa Semina hii kwani itasaidia kuwainua vijana kimaendeleo na kiuchumi.

Mgeni Rasmi Mh. Anthony Mavunde amewaasa Vijana wote waliohudhuria mafunzo hayo kwa siku tatu kuhakikisha wanayafanyia kazi yote waliyojifunza kwa vitendo. Aidha amemshukuru Mkufunzi ndugu Kenani Kihongosi ambaye pia ni M/Kiti wa UVCCM Mkoa wa Iringa kwa kujitolea kutoa mafunzo hayo kwa mda wa siku tatu na pia amemuahidi kuwa ipo siku atamuita kwenye jimbo lake ili atoe simina hii kwa kata zote.

Mh Anthony Mavunde  amesema mambo mengi ya muhimu mojawapo
 Natamani kuwaona Vijana wa Mkoa wa Mwanza, Mkoa wenye rasilimali za kutosha  uwe mfano wa kutosha kwa vijana wa mikoa mingine kwamba mnauwezo wa kupiga hatua kimaendeleo na kiuchumi.”
Pia
“Sisi na Ofisi ya Waziri Mkuu tumeandaa muongozo  ambao  kijana ambaye amemaliza chuo kikuu ukileta maombi ofisini kwetu  tunakusaidia kukutafutia  makampuni mbalimbali kutokana na fani uliyosomea,  anakwenda kujifunza kwa miezi 6 hadi 12  na badae atapewa cheti cha  kumtambua  hata akienda  kuomba kazi kampuni nyingne inakuwa rahisi kupata”

Aidha Mh Anthony Mavunde Amegawa Vyeti kwa kila wilaya ambazo zimehudhuria siku zote tatu.

Imetolea na
Katibu UVCCM Mkoa wa Mwanza











No comments:

Post a Comment