Monday, September 17, 2018

KONGAMANO KUBWA LA UJASIRIAMALI LAANZA LEO HAPA GHANDHALL JIJINI MWANZA


Umoja wa Vijana CCm Mkoa wa Mwanza Umeandaa kongamano kubwa la Ujasiriamali  litakalo fanyika kwa siku tatu(3)  kuanzia tarehe 17 – 19/09/2018.

Akizungumza M/kiti wa UVCCM Mkoa wa Mwanza  ndugu Jonas Rufungulo  ameelezea namna ambavyo kongamano litakavyo kuwa la aina yake. Ameeleza mambo ambayo vijana na wasio vijana  watakavyonufaika na semina hii kubwa ya Ujasiriamali, Moja ya mambo aliyoyaeleza ni pamoja na watu kujifunza mambo mengi kama vile kutengeneza batiki, vikoi pamoja na  ufungaji.

M/kiti wa UVCCM mkoa wa Mwanza ameeleza kuwa mgeni rasmi wa kufungua semina hii ni M/kiti wa UVCCM Taifa Mh. Kheri Denis James  na Tarehe 19/09/2018 ambapo itakuwa mwisho wa semina hii itafungwa na Mh Anthony Mavunde ambaye ni Naibu waziri  Vijana ajira  na kazi.

Aidha M/kiti wa UVCCM Mkoa  wa Mwanza amesisitiza watu waote kufika katika semina hii bila kuangalia chama, dini kabila na hata rangi, hii ni semina ya watu wote wakubwa kwa wadogo na hakuna kiingilio amesisitiza zaidi.

Aidha hadi sasa watu mbali mbali wameshaanza kujitokeza pamoja na viongozi mbali mbali wa UVCCM idara mbalimbali hapa jijini Mwanza miongoni ni Katibu wa UVCCM Mwanza Ndugu Odilia Batyomayo, M/kiti Mkoa Seneti Mkoa wa Mwanza Bi. Lwiza Mwenda, Katibu wa Wilaya ya Ilemela  Mh. Nehemia Philimon na Wengine weng.

Karibuni sana tujifunze Elimu ya Ujasiriamali.

Imetolewa na
Ofisi  ya  Katibu UVCCM Mkoa wa Mwanza



No comments:

Post a Comment