Sunday, October 14, 2018

MJUMBE BARAZA KUU UVCCM TAIFA -MWANZA NDG KASHILIMU JUMA RICHARD ASHIRIKI KATIKA KUADHIMISHA SIKU YA KIFO CHA BABA WA TAIFA NA MAMIA YA VIJANA WILAYANI SENGEREMA

14/10/2018 Mjumbe Baraza Kuu Uvccm Taifa aungana na mamia ya vijana katika kufanya usafi maeneo mbalimbali mjini Sengerema 

Sambamba na kufanya usafi Ndg Kashilimu Juma Richard ameshiriki katika zoezi la kuchangia damu kwani ni ishara ya uzalendo mkubwa na ni miongoni mwa vijana wachache wenye kufanya zoezi hili.

Kupitia zoezi hili ni ibada tosha kwani hata Mungu  anapenda na kuwainua wenye uwezo wa kujitoa kwa ajili ya kuokoa maisha ya ndugu zetu.

Wapo wahitaji wengi wa damu kama watoto  wa chini ya umri wa miaka 5, wanaopata ajali, lakini Wapo wanaotakiwa kuongezwa damu kutokana na matatizo mbalimbali

Kupitia zoezi hili tutaweza kupunguza vifo vya watoto na mama zetu wanaopoteza maisha na damu  vipindi vya kujifungua.

Mjumbe baraza kuu awataka vijana waendelee kujitoa hasa katika zoezi la kizalendo lenye tija kwa taifa na wananchi kwa ujumla.

Mwisho 
Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere atakumbukwa na ataendelea kukumbukwa kwa taifa,Africa na Dunia yote.
Mungu ampumzishe kwa amani 
Tanzania tunaumia kumpoteza shujaa ila kazi ya Mungu haina makosa

Kashilimu Juma Richard
Mjumbe baraza kuu uvccm Taifa












No comments:

Post a Comment